Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) amezidua wiki ya Elimu nchini iliyoanza tarehe 03 Mei hadi Mei 10, 2014 mjini Dodoma.
| |||||||||||||||||
Akizindua maadhimisho hayo Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuweka msingi wa dhati katika shule za kata kwa lengo la kupandisha kiwango cha kufaulu. Amesema maadhimisho hayo ni sehemu ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa – Big Results Now ( BRN ) katika Sekta ya Elimu ambayo yanafanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.
| |||||||||||||||||
Maadhimisho hayo yana lenga kuelimisha Umma wa Watanzania juu ya umuhimu wa Elimu Bora na ushiriki wao katika kuhakikisha kuwa elimu bora inapatikana kwa wote.
| |||||||||||||||||
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu yamejumuishwa pamoja na kuainisha, kuwatambua na kutoa Tuzo kwa Wanafunzi, Walimu, Shule, Halmashauri na Mikoa iliyofanya vizuri katika Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi na Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Sekondari Kidato cha 4 mwaka 2013.
| |||||||||||||||||
Kwa upande wa taarifa za Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne zinaonesha kuwa, ufaulu wa juu (Daraja la I-III) kwa mwaka 2013 unaonekana kuwa mkubwa ukilinganishwa na miaka ya 2010, 2011, na 2012 kwa shule za Kata, Serikali, Binafsi na Seminari. Aidha, idadi ya watahiniwa waliofaulu katika madaraja hayo nayo iliongezeka kwa aina zote za shule.
| |||||||||||||||||
Kwa upande wa Shule za Kata, Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa ufaulu wa Shule za Kata ni mdogo (Asilimia 48 ) ikilinganishwa na Asilimia 59.7 Shule za Serikali; Asilimia 84.3Shule Binafsi na Asilimia 80.8 Shule za Seminari. Hata hivyo, kwa idadi ya wanafunzi wengi waliofaulu katika Mitihani hiyo ni wa kutoka katika Shule za Kata ambao ni 109,229 ikilinganishwa na52,242 wa Shule za Binafsi, 33,533 wa Shule za Serikali na 6,149wa Shule za Seminari. Hii inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya Wanafunzi iko kwenye Shule za Kata.
| |||||||||||||||||
Aidha, takwimu zinaonesha kuwa, ufaulu usioridhisha wa Daraja la Sifuri wa Shule za Kata kwa mwaka 2013 ni wa chini kuliko miaka mitatu iliyopita.
| |||||||||||||||||
Kutokana na yaliyojitokeza kwenye matokeo hayo ya Kidato cha Nne mwaka 2013, ni dhahiri kwamba, Serikali inahitaji kuongeza uwekezaji kwenye shule zake za Kata na zile za Serikali kwa kasi zaidi pia kuna umuhimu mkubwa wa kuangalia upya uwekezaji kwenye shule za vipaji maalum ili kufikia malengo yayowekwa wakati wa kuanzishwa kwa shule hizo. Uwekezaji huo ulenge zaidi kwenye miundombinu, walimu, ukaguzi, vitabu, na vitendea kazi.
PICHA: Baadhi ya wanafunzi wakiwa wamekaa jukwaani wakati mgeni rasmi Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Kayanza Peter Pinda (MB) akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa wiki ya Elimu nchini inayofanyika kitaifa mjini Dodoma kauli mbiu ya mwaka huu inasema “ELIMU BORA KWA WOTE INAWEZEKANA, TIMIZA WAJIBU WAKO”
PICHA: Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda akipata maelezo katika banda la Chama cha Walimu Tanzania kushoto kwake ni Mhe.Kassim Majaliwa Naibu Waziri TAMISEMI (ELIMU) wa kulia kwake ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dk Shukuru Kawambwa.
|
Thursday, May 29, 2014
MAONESHO WIKI YA ELIMU DODOMA YAFANA
1:01 AM
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment